Tuesday, May 29, 2012

Zanzibar imechafuka!

VURUGU ZASHIKA KASI, DK NCHIMBI, IGP MWEMA WATOA MAAGIZO MAKALI KWA POLISI
Waandishi Wetu
VURUGU zilizozuka kuanzia juzi katika maeneo kadhaa ya Mji wa Zanzibar na kudhibitiwa, ziliibuka tena jana baada ya vijana kuchoma matairi ya magari barabarani wakipinga kurejeshwa rumande kwa Mhadhiri wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam Zanzibar (Jumiki), Sheikh Musa Juma Issa.

Awali, hali ya amani ilikuwa imerejea baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema jana kuongoza mkutano uliojumuisha taasisi mbalimbali visiwani Zanzibar kwa lengo la kutafuta suluhu ya machafuko hayo ambayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa mali.

Hata hivyo, muda mfupi baada ya mkutano huo uliomalizika kwa makubaliano ya kurejea kwa amani, vurugu ziliibuka tena.

Vurugu tena

Kurudishwa rumande kwa Sheikh Issa baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana mahakamani na wenzake wengine sita wakituhumiwa kuhusika na vurugu hizo kulichochea vurugu katika maeneo ya Amani na Mwanakeretwe kwa vijana kuchoma matairi na kufunga mitaa.

Vurugu hizo za vijana zilisababisha polisi kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya vijana hao ambao licha ya kupigwa mabomu walizidi kupiga kelele wakilaani Muungano.

Hadi jana jioni, maeneo ya Chumbuni, Amani, Mwembaladu hali ilikuwa bado tete huku polisi wakifunga barabara kwa ajili ya kudhibiti vijana hao.

Nchimbi, Mwema
Katika mkutano wao, Dk Nchimbi na IGP Mwema walikutana na viongozi wa taasisi za Kiislamu Zanzibar, wawakilishi wa Balozi za Marekani, Norway na Uingereza na kujadili masuala kadhaa ya kuleta amani visiwani humo.

Mkutano huo uliofanyika kwenye Makao Makuu ya Polisi Zanzibar uliwashirikisha pia maofisa wa sekta ya utalii.

Katika mkutano huo, Waziri Nchimbi alisema suala la kulinda amani ni la wote na akawataka viongozi wa dini na wanasiasa kuhakikisha Zanzibar inaendelea kuwa na amani.

“Kwa mwaka mmoja na nusu hivi sasa Serikali ya Umoja wa Kitaifa imefanya kazi nzuri na tunawapongeza viongozi wote kwa kazi hiyo; Rais Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wake wa Kwanza Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wake wa Pili, Balozi Seif Ali Idd, sasa tusiwavunje moyo,” alisema Nchimbi.

Alisema kuendelea kwa vurugu Zanzibar ni kuonyesha viongozi hao wameshindwa kazi jambo ambalo si sahihi na kwamba vurugu zinaweza kusababisha watalii kuondoka na hasa kwa kuzingatia msimu wa utalii unakaribia.

Nchimbi alisema ujio wake Zanzibar, ulilenga katika mambo matatu muhimu... “Kuwahakikishia Wazanzibari wote kuwa Jeshi la Polisi ni lao na litaendelea kuwalinda na kuwaeleza kuwa viongozi wote wa dini na siasa wana jukumu kubwa la kusaidia kujenga mazingira ya utulivu na amani Zanzibar.”

Aliliagiza jeshi hilo kuwatafuta na kuwachukulia hatua za kisheria watu wote waliohusika kufanya vurugu hizo ili haki itendeke.

Kwa upande wake, IGP Mwema aliahidi kushirikiana na viongozi wa taasisi za kidini ili kuendeleza amani na utulivu nchini. Alisema majadiliano na mazungumzo ni muhimu katika kuimarisha amani na kutatua migogoro iliyokuwapo akiahidi kuendelea kubaki Zanzibar.

Taasisi za dini
Kwa upande wake, kiongozi wa Umoja wa Kiislamu wa Elimu, Uchumi na Maendeleo (UKUEM), Dk Mohammed Hafidh Khalfan alilitaka Jeshi la Polisi kuepuka matumizi ya nguvu kubwa wakati wanapotekeleza majukumu yao.

Alisema taasisi yake pamoja na nyingine za Kiislamu zitatumia juhudi na busara za kuwafanya waumini wake waepuke vitendo vya fujo, kwani vinatoa fursa kwa wahalifu kufanya vitendo viovu.

Hata hivyo, katika kikao hicho Jumiki hawakushirikishwa na hivyo Dk Hafidh kushauri kuwa katika kikao hicho sauti za kundi hilo ni muhimu kusikika kwani baadhi ya mambo wangeweza kuyatolea maelezo.

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (Jumaza), Sheikh Muhidin Zubeir Muhidin ambaye alifanya juhudi za kuwasiliana na polisi na taasisi nyingine katika kutafuta suluhu za machafuko hayo aliahidi kuendelea na ushirikiano na wadau wote wa amani nchini.

“Sote tuna jukumu la kuhakikisha hali ya amani inarudi Zanzibar na Uislamu hautoi nafasi kwa kufanya uharibifu wala kumdhuru mtu,” alisema Sheikh Muhidin.

Mkurugenzi wa Utalii Zanzibar, Ali Khalil Mirza alisema sekta ya utalii inachangia pato kubwa la taifa kwa zaidi ya asilimia 75, inaweza kutetereka iwapo hali ya utulivu itatoweka visiwani humo na kushauri ushirikiano zaidi kati ya taasisi zote na wadau ili kuimarisha hali ya utulivu.

Marekani yajitosa

Ubalozi wa Marekani nchini umezitaka pande zote inazohusika kufanya kazi pamoja na kuhakikisha amani inapatikana visiwani humo.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt ilisema wanajua umuhimu wa mijadala ya kitaifa lakini ni muhimu pande zote zikitumia demokrasia na amani.

“Vurugu hizo zilizotokea kwa siku mbili zilizopita, zinachafua heshima ya Zanzibar ambacho ni kisiwa cha kwanza chenye amani ambacho kilifanya uchaguzi wenye mafanikio ulioleta Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema.

Alisema ni muhimu kulinda amani ya Zanzibar ambayo inaruhusu watalii na maendeleo ambayo ni muhimu kwa Wazanzibari na wageni kwa pamoja.

“Tunataka kila mmoja kulinda maisha na mali za watu wasiokuwa na hatia,” ilisema taarifa hiyo.

Kauli za mawaziri
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki alisema vurugu zinazoendelea visiwani Zanzibar, haziwezi kuzuia shughuli za Tume ya Katiba.
Alisema vyombo vya usalama vitahakikisha vinawakamata na kuwashughulikia wale wote waliohusika katika vurugu hizo.
Kairuki alisema mchakato mzima wa uanzishwaji wa tume hiyo ulifuata sheria na hakuna Katiba iliyovunjwa.
Wakati Kairuki akieleza hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan alisema hata kama kuna wananchi ambao hawataki Muungano, wanachotakiwa kufanya ni kutoa maoni kwa Tume ya Katiba.
“Wasubiri Tume ya Katiba itakapokuwa ikikusanya maoni ya wananchi waseme kuwa hawautaki Muungano lakini, si vinginevyo,” alisema.
Waziri huyo ambaye alionekana kutotaka kulizungumzia kwa kina suala hilo alihoji iweje aulizwe yeye. Alipoelezwa kuwa yeye ndio waziri anayehusika na masuala ya muungano alisema, “Wasubiri tu.
Kiongozi wa Kanisa
Akizungumzia vuguru hizo, Makamu Mwenyekiti wa Kanisa  Katoliki Parokia ya Mpendae, Geogre Suna alisema vijana hao walivamia kanisa hilo mnamo saa 8:15 kwa kufunga barabara na kisha kuingia ndani na kuanza kuchoma moto mabenchi ya kukalia waumini.
 
“Baada ya vijana kufika kanisani hapa mlinzi pamoja na fundi waliamua kukimbia kuokoa maisha yao, ndipo wakaanza kuchoma moto, kanisani na kuvunja vioo katika nyumba ya paroko,” alisema.
 
Katika eneo la Magomeni, vijana hao walivamia kiwanda cha mbao na kukichoma moto na kuchoma matairi na kuweka mawe makubwa barabarani hali iliyosababisha polisi kuwafukuza kwa kutupa mabomu mengi ya machozi pamoja na kupiga risasi.

Mtwara wanena

Wakazi wa Wilaya ya Tandahimba, Mtwara wamesema ili kumaliza kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni vyema kwa Katiba mpya ikafuta Zanzibar ili nchi hizo zitambulike kwa Tanzania bara na Tanzania Visiwani.
Wakichangia mada katika mdahalo wa kuwajengea uwezo na kuhamasisha wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kutoa maoni pindi Tume ya Katiba Mpya itakapofika wilayani humo, uliofanyika mjini Tandahimba mwishoni mwa wiki wananchi hao walisema ni wakati sasa kwa Katiba kumaliza kero hizo.

“Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kupata jina moja la Tanzania, iweje leo kuwepo Zanzibar? Hapa kunachotakiwa kuwapo ni Tanzania Bara na Tanzania Visiwani. Zanzibar na Tanganyika tulishaziua kwa kuunda Muungano,” alisema Gebra Msuya mkazi wa Tandahimba.

Monday, April 11, 2011

Mukama katibu mkuu mpya wa CCM

Chama cha mapinduzi (CCM) kimemteua ndugu Wilson Mukama katibu mkuu mpya wa CCM katika kikao chake kilichokuwa kinaendelea cha NEC.Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Yusufu Makamba baada ya kujiuzulu.wakati huo huo, Nape Nnauye pia ameteuliwa kuwa mkuu wa itikadi uenezi wa CCM huku mama Zakia Megji akichukua nafasi ya katibu-fedha

kama katibu mkuu mpya CCM

Chama cha mapinduzi (CCM) kimemteua ndugu Wilson Mukama katibu mkuu mpya wa CCM katika kikao chake kilichokuwa kinaendelea cha NEC.Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Yusufu Makamba baada ya kujiuzulu.wakati huo huo, Nape Nnauye pia ameteuliwa kuwa mkuu wa itikadi uenezi wa CCM huku mama Zakia Megji akichukua nafasi ya katibu-fedha.

Saturday, March 12, 2011

waandishi wambana spika makinda

KAULI ya Spika kutaka wabunge wasome magazeti kama barua, imemtia matatani baada ya waandishi wa habari jana kumtaka awaombe radhi kwanza, ili watekeleze ombi lake la kuvitaka vyombo vya habari, viwe kiungo kati ya Bunge na wananchi.

Hata hivyo Spika Anne Makinda, aligoma kuomba radhi na kwamba alitoa kauli hiyo katika mazingira ambayo, hakuamini kama vyombo vya habari vingeweza kutoa taarifa aliyodai kuwa haikumtendea haki.

Katika mkutano wa pili wa Bunge la Kumi mjini Dodoma, Makinda aliishambulia makala iliyoandikwa na gazeti hili kuhusu mabadiliko ya kanuni za Bunge, zilizogusa kambi ya upinzani bungeni ambayo wabunge waliitumia kama marejeo, akisema "magazeti yasomwe kama barua".

Lakini jana akifungua semina ya siku mbili ya waandishi wa habari za Bunge, makinda alibanwa na waandishi wakimtaka aombe radhi muda mfupi baada ya spika huyo kueleza kuwa vyombo vya habari, ni nguzo muhimu na kiungo kati ya Bunge na wananchi.

"Mheshimiwa spika leo umetaka vyombo vya habari viwe kiungo kati ya Bunge na wananchi, lakini katika Bunge lililopita uliwataka wabunge wasome magazeti kama barua ukimaanisha hayana umuhimu, unaweza kufuta kwanza kauli hiyo au kuomba radhi kabla hatujatekeleza ombi lako,," alihoji mmoja wa washiriki wa semina hiyo.


Akionekana kutaharuki Spika Makinda alijibu,"nilijua ntakumbana na swali hili na nimejiandaa vema, sio kuomba radhi bali kutoa ufafanuzi."Nilifedheheshwa na habari ile, waliandika kinyume na ilivyo, walisema mimi ninakandamiza upinzani. Hapana mimi natakiwa kutoegemea upande wowote kwani nikitenda yaliyoandikwa naweza kuvuruga amani ya nchi. Spika peke yake anaweza kuvuruga amani ya nchi," alisema

Spika Makinda alifafanua kuwa kilichofanyika haikuwa kubadili kanuni za Bunge bali kutafsiri.

"Tulitafsiri kanuni ya 14(2) ambayo inasema kambi rasmi ya upinzani inaundwa na wabunge wote wa upinzani. Zamani ilikuwa kambi rasmi ya upinzani inatengenezwa na asilimia 30 ya wabunge, lakini hili halijawahi kutekelezeka kwa kuwa mwaka 1995 wabunge wa upinzani walikuwa 46 ambao ni chini ya asilimia 30 na mwaka 2000 hawakufikia hata asilimia 2. Bunge likalazimika kubadilisha kanuni na kuwa asilimia 12.5 ya wapinzani inaweza kuunda upinzani," alifafanua.

Lakini akitoa mada katika semina hiyo mwandishi nguli wa habari, Jenerali Ulimwengu, alisema kuwa kauli ya Spika kutaka wabunge wasome magazeti kama barua ni makosa."...Kwa maoni yangu Spika Makinda aliposema wabunge wasome magazeti kama barua alikosea," alisema Ulimwengu.Katika semina hiyo Spika Makinda alisema kuwa kanuni za Bunge zitafanyiwa mabadiliko makubwa katika kipindi hiki cha bunge la kumi.

"Tunaenda kufanya mabadiliko makubwa ya kanuni, na hivyo kambi rasmi ya upinzani haitakuwa tena issue ya kuumiza kichwa..," alisema Makinda.Alisema pia kwamba katika Bunge lijalo Sheria ya Vyombo vya Habari inatarajiwa kufikishwa bungeni tayari kujadiliwa na kwamba wadau watapata nafasi ya kushiriki katika mijadala yake.

Kuhusu Katiba, Makinda alisema mchakato huo ni muhimu na kwamba vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kuwaelimisha na kuwapa taarifa wananchi kuhusu mabadiliko hayo ili nao washiriki katika uandikaji katiba hiyo mpya.

Thursday, March 10, 2011

Pengo: Sioni tatizo la maandamano ya Chadema

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amesema haoni tatizo katika maandamano yanayofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi jana, Kardinali Pengo alisema badala yake Serikali: “Ichimbue mizizi ya matatizo badala ya kukimbilia kukata matawi.”

Kauli ya Pengo ni kama inaunga mkono matamshi yaliyotolewa juzi na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliishauri Serikali kutotumia vyombo vya dola dhidi ya Chadema na badala yake ijirekebishe kwa kuwa na wepesi wa kukabiliana na matatizo yaliyopo nchini.

Kadhalika, kauli hiyo ya Pengo imekuja wakati Serikali ikiendelea kulaani maandamano hayo ya Chadema na kutaka yasitishwe kwa madai kuwa yanaweza kuleta machafuko nchini.

Katika mahojiano hayo Kardinali Pengo alisema haoni kama Chadema kinafanya vurugu katika maandamano yake kama baadhi ya watu wanavyodai: “Sioni ‘point’ ya kusema maandamano ya Chadema yanaweza kusababisha vurugu,” alisema Kardinali Pengo na kuongeza:

Alisema ikiwa kuna tatizo katika maandamano hayo kama inavyoelezwa na serikali, ni bora hali hiyo ikafafanuliwa mapema na kukiambia Chadema kisitishe kuandamana.

“Lakini serikali isichukulie ‘comment’ (maoni) ya mtu mmoja mmoja na kusema kwamba Chadema inasababisha vurugu, bila kusikiliza na kuchambua kwa undani,” alisema.

Aliongeza kuwa endapo serikali imechunguza na kubaini ukweli kwamba maandamano hayo yanaweza kuleta vurugu za kisiasa, basi iyasitishe badala ya kutoa kauli tu kwamba yanahatarisha amani.

Pengo alisema huenda uamuzi wa Chadema kufanya maandamano unatokana na madai yao dhidi ya kupanda kwa gharama za maisha, umeme na malipo kwa kampuni ya kufua umeme ya Dowans kwamba hayakusikilizwa.

Alisema Serikali haitakiwi kuyafumbia macho matatizo ya kisiasa nchini badala yake itafute kiini chake na namna ya kuyatatua.

“Serikali ianze kuchimbua mizizi ya matatizo ya kisiasa yaliyopo ndani ya Taifa, badala ya kukimbilia kukata matawi. Kwa sababu kuanza kukata matawi ni kuzidi kuipeleka nchi katika machafuko ya kisisasa na matokeo yake ni kuleta madhara kwa wananchi,” alisema.

Askofu huyo mkuu pia alisisitiza kuwa Serikali inatakiwa kuhakikisha inafuatilia matatizo yanayowakabili wananchi kwa sasa, ambayo yanahitaji ufumbuzi wa haraka ili watu wasipate fursa ya kudai mambo hayo kwa maandamano.

Kwa mujibu wa Kardinali Pengo, Serikali pia haipaswi kutoa vipaumbele kwenye masuala ya siasa na kusahau matatizo ya wananchi kwani hilo linaweza kuwa kiini cha vurugu... "Serikali iguswe kama ilivyoguswa na matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyotoka mwaka huu."


Baadaye akihubiri katika Misa ya Jumatano ya Majivu kuashiria kuanza kwa siku 40 za Mfungo wa Kwaresma ambao Wakristo hukumbuka mateso ya Bwana wao, Yesu Kristo kabla ya Pasaka zaidi ya miaka 2000 iliyopita, Kardinali Pengo alikemea tabia ya viongozi kung'ang'ania madaraka na kudhani kuwa bila wao nchi zao haziwezi kuwepo au kusonga mbele.

"Yapo matatizo katika viongozi wanaong'ang'ania madaraka wakiwa tayari hata kumwaga damu ya wengine ili wao wabaki madarakani. Hawa ni viongozi wanaofikiri uwezo unaweza kuwa ndani yao, wanajifanya wao Mungu," alisema Pengo.

Alisema viongozi hao wanatazama fadhila za kibinadamu wakiacha upungufu wao na kudhani kuwa wasipokuwa na madaraka basi nchi zao hazitakuwepo jambo ambalo si sahihi na halifai katika jamii.

"Viongozi hao wanajifanya wao ndiyo miungu, wanatazama fadhila za kibinadamu, wakiacha mapungufu yao. Hicho ni kiburi, wakumbuke kuwa Mungu aliwaumba kwa vumbi na watarudi kuwa vumbi, sasa kwa nini mnakuwa na kiburi?," Alihoji Kardinali Pengo na kuongeza;

"Mungu aliwaumba kwa vumbi kwa nini wawe na kiburi? Unadhani ukifa na nchi itakufa, kwani kabla yako nchi haikuwepo? Kumbuka wewe ni uvumbi na utarudi mavumbini."

Alisema thamani ya mtu haitokani na anavyojiona, bali nguvu ya Mungu akiwakumbusha Wakristo kutubu na kumrudia Mungu katika kipindi hiki cha Kwaresma.

Wakati huohuo; Festo Polea anaripoti kuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam ambao wapo katika taasisi isiyo ya kiserikali ya Truya wamesema ili kuondokana na machafuko yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani, viongozi wanaokiuka matakwa ya uongozi, uvunjaji wa Katiba na sheria za nchi wanapaswa kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Helman Sheluleta alisema Ibara ya 18 ya Katiba ya nchi inatambua haki ya mtu kutoa maoni, kusikilizwa na kuandamana kwa amani na kwa mujibu wa sheria lakini sheria inapovunjwa kwa ajili ya kupata haki ndiko kuhatarisha amani ya nchi.

Sunday, March 06, 2011

Sumaye: CCM ijibu hoja za Chadema

ASEMA KUIACHIA SERIKALI NI MAKOSA
WAKATI CCM ikitaka dola ikidhibiti Chadema, Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya tatu, Fredrick Sumaye, amekitaka chama hicho tawala kukabiliana na hoja za Chadema kisiasa badala ya kuiachia Serikali ipambane nao.Juzi CCM kilisema nyendo za Chadema zina agenda ya siri ya kuking’oa madarakani kwa kutumia nguvu kinyume cha katiba hivyo kiliitaka Serikali na vyombo vya dola kuchukua hatua za kisheria haraka.

“CCM inaviomba vyombo vya dola viwe imara kuchukua hatua za kisheria… Wanachofanya Chadema ni kutuchonganisha na wananchi, kutoa kauli hatari za kujaribu kughilibu akili za watu ili kuchochea machafuko, umwagaji wa damu na uasi. “Wanachochea wananchi wakisema, ‘peoples’ na hujibu ‘power’! (nguvu ya umma), Je mpo tayari kufanya kama Tunisia, Misri? (ambako serikali zilipinduliwa kwa nguvu ya umma)” alisema Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM, Itikadi na Uenezi, John Chiligati kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika juzi, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili bila kujua kwamba CCM wangekuwa wanazungumzia suala hilo, Sumaye alisema CCM inatakiwa kukabiliana kisiasa na hoja za Chadema na si kuiachia Serikali ipambane nao.

Kwa mujibu wa Sumaye, kazi ya siasa ni ya chama na si serikali, hivyo CCM wanapaswa kuwa mstari wa mbele kupambana na Chadema kwa sera na kujibu hoja zao zote ili kuongeza imani ya wananchi kwa chama hicho.Sumaye alisema si ishara nzuri kwa CCM kukaa kimya wakati wapinzani wanaendelea kukishtaki kwa wananchi kuwa kimeshindwa kufanya kazi.

Sumaye ambaye Mwananchi Jumapili ilimtafuta kusikia maoni yake kuhusu mfululizo wa mikutano ya Chadema na mustakabali wa CCM, alisema chama hicho tawala kinapaswa kujibu hoja zote za Chadema kisiasa na kama hakina majibu kiiombe Serikali majibu hayo na iyatoe kwa wananchi.

“Wale (Chadema) wanafanya kazi za siasa na hawa (CCM) wamekaa kimya, wanaiachia Serikali ndio inatoa majibu, hali hiyo si nzuri, chama kinapaswa kujibu hoja zote na kama hakina majibu, kiombe kwa serikali,” alisema Sumaye.Mjadala wa uhalali wa mikutano na maandamano ya Chadema uliibuliwa na Rais Jakaya Kikwete alipolihutubia taifa kupitia radio na televisheni Februari 28, mwaka huu na kuwaleza wananchi kuwa chama hicho cha upinzani kina lengo la kuleta machafuko nchini.

Rais Kikwete alisema hayo alipokuwa akilihutubia taifa mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.Kauli hiyo ya Rais Kikwete ambaye Chadema waliipuuza, ilisisitizwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Steven Wassira, aliyesema kuwa Chadema wasije kuilaumu serikali ikikosa uvumulivu na kuanza kutumia dola kukishughulikia.

Akihojiwa na gazeti hili Sumaye hakuishia kuishauri CCM kuja na hoja za kisiasa kujibu mapigo ya Chadema, bali pia alieleza aina ya watu wanaofaa kukiongoza chama hicho tawala wakati huu wa mabadiliko makubwa ya kisiasa.Sumaye alisema CCM inahitaji viongozi waadilifu, wachapakazi na wasio waoga kumshauri rais ili kuwa na mabadiliko ya kiutendaji yanayoendana na joto la kisiasa lililopo. “Tunahitaji viongozi wasioogopa kumshauri rais juu ya masuala mbalimbali, kama utakuwa na viongozi waoga, lazima kutakuwa na matatizo,” alisema Sumaye.

Kuhusu mabadiliko ndani ya CCM ambayo Rais Kikwete alisema ni lazima yafanyike, Sumaye alisema anakubaliana msimamo huo na anampongeza Rais kwa kutambua kuwa chama kinahitaji mabadiliko makubwa ya kiutendaji.“Kwanza nampongeza Mwenyekiti, maana ameona hilo. Watu wengi wanaona kuna umuhimu chama kurekebishwa na eneo muhimu ni utendaji wa viongozi wa ngazi mbalimbali ndani ya chama,” alisema Sumaye.

Sumaye alieleza kuwa CCM kitaendelea kushika dola, lakini kama kinataka hayo yatimie, mabadiliko ndani ya chama ni muhimu.Alisema umuhimu wa CCM kujifanyia tathmini ya utendaji ulianza kujionyesha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ambapo ikilinganishwa na chaguzi nyingine, chama kilipata upinzani mkali."Sasa ni dhahiri kunahitajika mikakati madhubuti ili kuhakikisha mwaka 2015 unakuwa mrahisi kwa CCM," alisema Sumaye.

Ndejembio atabiri anguko
Habel Chidawali anaripoti kutoka Dodoma kuwa, Kada maarufu wa CCM, Pancras Ndejembi amekitabiria chama hicho kikongwe kuzama.Kada huyo ambaye ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Dodoma alisema jana kuwa hali ilipofikia kwa sasa, CCM inaonekana kupoteza mwelekeo na kutia shaka mustakbali wa chama hicho siku za usoni.

Ndejembi ambaye aliwahi kutumikia nyadhifa mbalimbali ndani ya serikali na chama katika utawala wa Serikali ya awamu ya kwanza, alisema CCM bado haijaingia shimoni ila inaelekea huko.“Ni kweli chama hakifuati utaratibu uliokuwepo ndio maana nasema kuwa kinaelekea kuzama tofauti kabisa na enzi zetu ambapo Mwalimu Julius Nyerere alikuwa anasisitiza kuwa turudi kwa wanachama tukae nao na kuzungumza, jambo ambalo sasa hilo halipo na viongozi wamebaki huko juu,” alisema Ndejembi.

Alisema viongozi wa ngazi ya taifa wamebaki katika maofisi yao na kushindwa kurudi katika ngazi za chini kuimarisha chama na matokeo yake wanaishia kupiga kelele bila ya kuwa na uhakika wanachama ngazi ya chini wanataka nini.Ndejembi hivi alisema hakuna mshikamano wa dhati ndani ya chama jambo linalowafanya wanachama kumuachia mzigo wote Mwenyekiti wa Taifa.

“Watu wanaishia kulaumiana kila kona kwamba chama kimefanya nini, mara wanasema bado kimesimama wengine wanasema kuwa kinayumba, ila ukweli utabaki palepale kuwa CCM tunazama sasa,” alisisitiza.Kuhusu nguvu ya wazee ndani ya Chama Ndejembi alisema: “Sisi tumestaafu hivyo tupo tupo na kama hawataki kutuita unadhani tutakwenda ? Lakini, wakisema tuende tuko tayari kukaa pamoja nao kutengeneza utaratibu wa kukinusuru chama kisizame kabisa katika tope”.Ushauri

Kuhusu nini kifanye ili kukinusufu CCM, alisema unahitajika mshikamano wa dhati kati ya viongozi na wanachama: “viongozi wanahitaji kutambua kwa dhati kuwa chama kiko ngazi ya chini kuanzia kwa wajumbe wa nyumba kumi sio ngazi ya mikoa”.Alishauri kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa anatakiwa abaki kama kiongozi wa kutoa ushauri kwa juu, lakini awe na watu wanaochukua mawazo kutoka kwa wanachama wa ngazi ya chini.

Hata hivyo, alisema viongozi wa taifa bado wana mfumo mbovu wa mawasiliano, kwani kila mtu katika nafasi ya juu ni msemaji, jambo linalofanya wajichanganye katika taarifa zao.

Friday, March 04, 2011

Kafulila: Tuko pamoja na Chadema

CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimesema maandamano na migomo inayotokea nchini inasababishwa na serikali kushindwa kutatua kero za wananchi na kwamba hayasababishwi na chama chochote cha siasa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa Habari na Uenezi wa chama hicho, David Kafulila alisema wanaosema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinachochea vurugu siyo kweli.

Kafulila alitoa kauli hiyo siku chache baada ya wanachama wa Chadema kuandamana mjini Mwanza, na baada ya siku mbili, Rais Jakaya Kikwete alihutubia taifa na kusema kwamba Chadema kinataka kuleta machafuko kwa kudai mambo yasiyotekelezeka.

“Kazi wanayoifanya Chadema sioni kama ina tatizo, mimi tunatofautina na Chadema, lakini si kwa kila jambo, wanaosababisha maandamano siyo Chadema, NCCR wala CUF ni wananchi kwa sababu serikali imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili,” alisema Kafulila.

Alisema iwapo wanafunzi vyuoni wangepata mikopo yao kwa wakati, wafanyakazi kulipwa mishahara mizuri pamoja na mambo mengine kutekelezwa kwa wakati hakuna Mtanzania ambaye angelalamika wala kuandamana.


“Tatizo la umeme sio la chama ni la wananchi, hata sisi NCCR tuko tayari kwa lolote, tutaanza kazi kama wanayoifanya Chadema, lengo letu sote ni kuhakikisha wananchi wanapata haki zao na si kupika chuki katika jamii,” alisema Kafulila.

Alisema licha ya Tanzania kuwa nchi ya saba duniani kwa kupata misaada, lakini kila kukicha inazidi kurudi nyuma kimaendeleo.

“Tanzania ni ya saba kwa kupewa misaada, halafu wananchi wakiandamana vinasingiziwa vyama vya siasa kuwa ndio chanzo,”alisema.

“Hatuipingi Chadema, siipingi Chadema, NCCR tunajipanga kuwasha moto kuamsha watanzania waiwajibishe serikali yao, pale inaposhindwa kutatua matatizo bila sababu,” alisema Kafulila

Wednesday, July 14, 2010

Paul the octopus could make millions

International icon and unofficial king of Spain, Paul the Oracle Octopus has officially retired from the World Cup match-predicting racket and may now be used to cash in. According to CNN, the Sea Life aquarium where Paul resides is entertaining offers for Paul's promotional services and PR people are drooling over his potential to make millions.
best known for generating tabloid headlines such as "Freddie Starr ate my hamster," believes Paul, who was born in England, has ended his soothsaying days at exactly the right time. "Obviously his 100 percent record is remarkable but the minute he gets it wrong it all disappears," Clifford told CNN.
Now Paul could star in light-hearted commercials. "If you get it right, and remember Paul has had worldwide success ... you're talking about an earning potential of £2 or £3 million (up to $4.5 million), maybe more. It's got to bring a smile to everybody's face. You've got the world's first multimillion-pound octopus here.
Up to $4.5 million for the endorsement of an octopus that ate a clam out of a box labeled with the flag of a match-winning team eight consecutive times? It's ridiculous, but when you consider the money paid to humans who have done far less than that to endorse a wide range of horrible products, it starts to make sense.
[Video: Watch the octopus in action]
The only problem with Paul? He's just six months shy of the average three-year lifespan for an octopus. Then again, that's probably a generous assessment of how long people will remember him anyway.
Another expert agreed, saying there was no limit to the ways in which Paul could be marketed. "Obviously he has a short shelf life but there are many options," said Allyson Stewart-Allen, director of London-based International Marketing Partners.
"A good use for him would be in adverts featuring two competing brands, such as Coke or Pepsi. Which does Paul prefer?" said Stewart-Allen.
"The gaming industry would be the logical use for Paul, or marketing a service that compares the market. Or he could just be an icon, marketing a company like Octopus Travel, for instance.
So keep an eye out for Paul the octopus billboards, TV ads and Happy Meal toys over the coming months. Followed by the most expensive octopus dish ever.

Followers